• Malalamiko |
    • Mawasiliano |
    • Maswali yanayoulizwa mala kwa mala |
    • Barua Pepe za watumishi |
    • Gallery |
Halmashauri ya Wilaya ya Momba
Halmashauri ya Wilaya ya Momba

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Momba District Council

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Wasifu
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha
      • Kilimo
      • Idara ya Sekondari
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Utawala na Utumishi
      • Shughuli za Kiuchumi na Uzalishaji
      • Planing stastistics and Monitoring
      • Mifugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Tehama
      • Bee Keeping
      • Election
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Fishing
  • Madiwani
    • Councilors List
    • Kamati Za Kudumu
      • Fedha Na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwnyekiti
    • Tatiba za Vikao
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
      • Miradi inayoendelea
    • Ongoing Project
  • Matangazo
    • Miongozo
    • Procedures
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Library For Costumer Service
    • Strategics Plan
  • Kituo cha Habari
    • Press Release
    • Video
    • Matamko
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Gallery

Kilimo

  • KILIMO:

Shughuli kuu ya kiuchumi kwa wakazi wa wilaya ya Momba ni Kilimo ambapo asilimia 80 ya wakazi hutegemea kilimo. Katika kilimo, fursa zilizopo katika mazao ya kilimo ni kama ifuatayo:-

  • Kilimo cha mpunga katika maeneo ya Iyendwe, chitete, kamsamba , mkulwe, chilulumo, msangano.
  • Eneo lililotengwa ni Hekta 13,466 zenye uwezo wa kuzalisha Tani 37,783 kwa mwaka.
  • Kilimo cha mtama katika maeneo ya msangano, mkulwe, chilulumo, kamsamba, mpapa, ivuna, mkomba.
  • Eneo lililotengwa ni Hekta 13,015 zenye uwezo wa kuzalisha Tani 20,515 kwa mwaka.
  • Eneo la umwagiliaji Naming’ongo .
  • Eneo lina ukubwa wa Hekta 1,500 zenye uwezo wa kuzalisha Tani 9,000 za mpunga kwa mwaka
  • Kilimo cha miwa katika kata ya kapele
  • Eneo lina ukubwa wa Hekta 1,752.
  • Kilimo cha kahawa katika tarafa ya Ndalambo
  • 2.1.1 MAZAO MAWILI MUHIMU YENYE KULETA MATOKEO YA HARAKA KATIKA KUBORESHA KIPATO CHA WANANCHI WA MOMBA

Pamoja na Halmashauri ya Wilaya ya Momba kuwa na fursa nyingi kama ilivyoainishwa hapo juu, mazao ya Mpunga na Mtama yanaweza kuleta matokeo ya haraka kwa wananchi katika kuinua kipato chao na kuwa malighafi za uhakika katika kuanzisha viwanda vya kusindika mazao hayo. Hii itasaidia kuongeza mnyororo wa thamani wa mazao hayo.

2.1.2 KWA NINI MPUNGA NA MTAMA

Mpunga

  • Ardhi ya Momba ina udongo wenye rutuba inayostawisha zao la mpunga kwa wingi katika maeneo ya Kata za Kamsamba, Ivuna, Mkomba, Chilulumo, Mkulwe na Kapele na upatikanaji wa soko la uhakika. Maeneo haya yana jumla ya wakulima wa mpunga 19,877. Eneo linalofaa kwa kwa kilimo cha mpunga ni hekta 13,466 zenye uwezo wa kuzalisha Tani 37,783 kwa mwaka.
  • Uwepo miundombinu ya Kilimo cha umwagiliaji katika eneo la Naming’ongo ambayo itasaidia kutoa ajira kwa wakulima wapatao 7,500 kutoka hatua ya uzalishaji hadi usindikaji na masoko. Eneo linalofaa kwa umwagiliaji ni hekta 5,000 kwa sasa eneo lenye miundombinu ya umwagiliaji ni hekta 1,500. Uzalishaji Kwa mwaka unatarajiwa kufikia tija ya tani 6 kwa Hekta, hivyo kutoa jumla ya tani 9,000 kwa Hekta 1,500 zilizopo katika eneo la umwagiliaji.

Mtama

  • Ardhi ya Momba ina udongo wenye rutuba inayostawisha zao la mtama kwa wingi katika maeneo ya Msangano, Chitete, Mkulwe, Chilulumo, Kamsamba, Mpapa, Ivuna, Mkomba na upatikanaji wa soko la uhakika. Maeneo haya yana jumla ya wakulima wa mtama 4,306 na eneo linalofaa kwa kilimo cha mtama ni hekta 13,015 zenye uwezo wa kuzalisha Tani 20,515 kwa mwaka. Pia zao hili lina uwezo mkubwa wa kustahimili ukame na hivyo basi kufanya zao hili liwe la uhakika kwa kuwa huhitaji mvua kidogo.

2.1.3 JITIHADA ZILIZOFANYIKA

  1. MPUNGA

Halmashauri kwa kushirikiana na wananchi pamoja na Umwagiliaji kanda ya Mbeya imejenga Skimu ya umwagiliaji ya Naming’ongo kwa ajili ya zao la mpunga. Kwa sasa eneo lenye miundombinu ya umwagiliaji ni hekta 1,500 zinazolimwa. Uzalishaji Kwa mwaka unatarajiwa kufikia tija ya tani 6 kwa Hekta, hivyo kutoa jumla ya tani 9,000 kwa Hekta 1,500.

Pia halmashauri kupitia mradi wa SAGCOT-CTF unaotekelezwa na Kampuni ya Mtenda imetoa mafunzo kwa wakulima 41 kuhusu kilimo cha biashara na elimu ya ujasriamali. Mradi tayari umeajiri Afisa Kilimo Mmoja ambaye atashughulikia utekelezaji wa mradi huo katika wilaya ya Momba eneo la Naming’ongo.

Halmashauri kupitia mradi wa MIVARF imewezesha uanzishwaji wa vikundi 76 katika kata nne za Ivuna, Mkomba, Chilulumo na Mkulwe na chama kimoja cha ushirika katika kata ya Kamsamba. Vikundi hivi vina jumla ya wakulima 1,835 ikiwemo wanawake 1,004 na wananume 831 wanaojishughulisha na kilimo cha mpunga. Vikundi hivi vinalima jumla ya hekta 1,944 ambazo huzalisha tani 4,747.68 kwa mwaka.

  1. MTAMA

Halmashauri kuanzia mwaka 2015 imehamasisha wananchi kulima zao la mtama kwa kuwa zao hili lina soko la uhakika na Uhakika wa kuvuna upo kwa vile linavumilia ukame.

Katika mavuno ya msimu wa 2015/16 halmashauri iliwaunganisha wakulima na kampuni ya Rapha group ambayo ilinunua tani tani 1,200 za mtama katika Halmashauri ya Wilaya ya Momba.

Aidha Halmashauri imefanya mazungumzo ya kuwaunganisha wakulima wa zao la mtama kwenye kilimo cha mkataba na kampuni ya OBO investment ambayo ipo tayari kununua tani 15,000 za mtama.



Matangazo

  • MAJINA YA WANAFUNZI WALIOPANGIWA KIDATO CHA KWANZA 2023 December 13, 2022
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI YATANGAZWA January 04, 2023
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE January 28, 2023
  • ORODHA YA MAJINA WALIYOITWA KWENYE USAHILI WA ZOEZI LA SENSA July 18, 2022
  • View All

Taarifa Mpya

  • MAAFISA UGANI NA WATENDAJI WA KATA WAGAWIWA PIKIPIKI ZENYE THAMANI YA TSH MIL 159 ILI KURAHISISHA UTOAJI WA HUDUMA KWA WANANCHI.

    March 09, 2023
  • BILION 2 KUKUSANYWA KUTOKA KATIKA VYANZO VYA NDANI KWA MWAKA WA FEDHA 2023/2024

    January 24, 2023
  • KAMATI YA YA SIASA YA WILAYA IMEFANYA UKAGUZI WA MIRADI YA MAENDELEO LEO TAREHE 16 NOVEMBA 2022

    November 16, 2022
  • MIKAKATI KUKABILIANA NA WIMBI LA UDUMAVU MOMBA

    November 09, 2022
  • View All

Video

UKODISHAJI WA MAGHALA -MOMBA DC
Picha za video

Linki za Haraka

  • You tube
  • Plan Rep Link
  • FFARS Online Docomentation
  • FFARS Link
  • KIBALI CHA KUSAFIRI NJE YA NCHI

Tovoti Mashuhuri

  • Utumishi
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani
  • Wizara ya Kilimo
  • http://www.tasaf.go.tz/

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Mawasiliano

    Tunduma-Momba

    Anwani: S.L.P 273 Tunduma Momba

    Namba ya Simu: 0252957476

    Simu: 025 295 7476

    Barua Pepe: ded@mombadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mala kwa mala
    • Ramani
    • Huduma

Haki zote zimeifadhiwa ©2018 Momba dc